5 January 2015

AUNTY EZEKIEL...!!! APEWA SOMO NA FLORA MVUNGI

njiwa
 
Siku chache baada ya kunasa mimba ya pili, mwigizaji Flora Mvungi amempa somo la uzazi staa mwenzake, Aunt Ezekiel kuwa anapaswa kuzingatia taratibu za kliniki, vinginevyo atapata madhara makubwa.


Staa wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel.

Akizungumza na mwanahabari wetu, Flora alisema mbali na kupunguza kujirusha, anamshauri Aunt aende kwa Dokta Fadhili Emily wa Kliniki ya The Fadhaget Sanitarium Kitengo cha Sayansi na Tiba iliyopo Mbezi Beach- Africana jijini Dar kwani walimsaidia sana yeye katika kumuelekeza namna ya kulea mimba hadi kujifungua akiwa salama.

Alisema wataalam hao walimsaidia katika mimba yake ya awali na hata hii ya pili wanaendelea kumpa tiba ya sayansi asilia hivyo kama Aunt ataamua kumsikiliza na kufuata ushauri wa kutopenda starehe na kuvaa viatu virefu basi atajifungua salama.

Dokta Fadhili Emily wa Kliniki ya The Fadhaget Sanitarium Kitengo cha Sayansi na Tiba.
“Kuna dawa ambazo unapewa kuanzia hatua za awali, kamwe huwezi kutematema mate hovyo kama wajawazito wengine, mtoto anakua vizuri na hadi unafikia hatua ya kujifungua huwezi kupata kashikashi,” alisema Flora ambaye ni mke wa staa wa Bongo Fleva, Hamis Ramadhan ‘H.Baba’.
Aunt ambaye kwa sasa tumbo linaonekana kuwa kubwa, amekuwa akionekana katika kumbi za starehe akijirusha akiwa na mavazi ya kihasara hali ambayo inaelezwa kuwa huenda ikamsababishia madhara kiafya.
njiwa2

Like Page Yetu Hapa Kuungana Nasi Facebook